3. Je! Siyo msiba kwa wasio haki,Na hasara kwao watendao uovu?
4. Je! Yeye hazioni njia zangu,Na kuzihesabu hatua zangu zote?
5. Kwamba nimetembea katika ubatili,Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;
6. (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa,Ili Mungu aujue uelekevu wangu);
7. Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia,Na moyo wangu kuyaandama macho yangu,Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;
8. Basi na nipande, mwingine ale;Naam, mazao ya shamba langu na yang’olewe.
9. Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke,Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;
10. Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine,Na wengine na wainame juu yake.
11. Kwani hilo lingekuwa kosa kuu;Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;
12. Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu,Nao ungeyang’oa maongeo yangu yote.