Ayu. 3:2-11 Swahili Union Version (SUV)

2. Ayubu akajibu, na kusema;

3. Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi,Na ule usiku uliosema,Mtoto mume ametungishwa mimba.

4. Siku hiyo na iwe giza;Mungu asiiangalie toka juu,Wala mwanga usiiangazie.

5. Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake;Wingu na likae juu yake;Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.

6. Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu;Usihesabiwe katika siku za mwaka;Wala kutiwa katika hesabu ya miezi.

7. Tazama, usiku huo na uwe tasa;Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe.

8. Na waulaani hao waulaanio mchana,Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani.

9. Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza;Na utafute mwanga lakini usiupate;Wala usiyaone makope ya asubuhi;

10. Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu.Wala kunifichia taabu machoni.

11. Mbona si kufa mimi tokea mimbani?Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni?

Ayu. 3