Ayu. 3:15-19 Swahili Union Version (SUV)

15. Au pamoja na wakuu wenye dhahabu,Waliozijaza fedha nyumba zao;

16. Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako;Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa.

17. Huko waovu huacha kusumbua;Huko nako hao waliochoka wapumzika

18. Huko wafungwa waona raha pamoja;Hawaisikii sauti yake msimamizi.

19. Wakuu na wadogo wako huko;Mtumishi yu huru kwa bwana wake.

Ayu. 3