Ayu. 29:14-18 Swahili Union Version (SUV)

14. Nalijivika haki, ikanifunika,Adili yangu ilikuwa kama joho na kilemba.

15. Nalikuwa macho kwa kipofu,Nalikuwa miguu kwa aliyechechemea.

16. Nalikuwa baba kwa mhitaji,Na daawa ya mtu nisiyemjua naliichunguza.

17. Nami nilizivunja taya za wasio haki,Na kumpokonya mawindo katika meno yake.

18. Ndipo niliposema, Nitakufa ndani ya kioto changu,Nami nitaziongeza siku zangu kama mchanga;

Ayu. 29