Ayu. 28:4-11 Swahili Union Version (SUV)

4. Hufukua shimo mbali na makao ya watu;Husahauliwa na nyayo zipitazo;Huning’inia mbali na watu, huyumba-yumba huko na huko.

5. Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula;Na chini yake hupinduliwa kama kwa moto.

6. Mawe yake ni mahali zipatikanapo yakuti;Nayo ina mchanga wa dhahabu.

7. Njia ile hapana ndege mkali aijuaye,Wala jicho la tai halijaiona;

8. Wanyama wakali wajivunao hawajaikanyaga,Wala simba mkali hajaipita.

9. Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake;Huipindua milima hata misingi yake.

10. Hukata mifereji kati ya majabali;Na jicho lake huona kila kito cha thamani

11. Hufunga vijito visichuruzike;Na kitu kilichostirika hukifunua.

Ayu. 28