11. Hufunga vijito visichuruzike;Na kitu kilichostirika hukifunua.
12. Bali hekima itapatikana wapi?Na mahali pa ufahamu ni wapi?
13. Mwanadamu hajui thamani yake,Wala haionekani katika nchi ya walio hai.
14. Vilindi vyasema, Haimo ndani yangu;Na bahari yasema, Haiko kwangu.
15. Haipatikani kwa dhahabu,Wala fedha haitapimwa iwe thamani yake.