Ayu. 28:11-15 Swahili Union Version (SUV)

11. Hufunga vijito visichuruzike;Na kitu kilichostirika hukifunua.

12. Bali hekima itapatikana wapi?Na mahali pa ufahamu ni wapi?

13. Mwanadamu hajui thamani yake,Wala haionekani katika nchi ya walio hai.

14. Vilindi vyasema, Haimo ndani yangu;Na bahari yasema, Haiko kwangu.

15. Haipatikani kwa dhahabu,Wala fedha haitapimwa iwe thamani yake.

Ayu. 28