1. Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2. Jinsi ulivyomsaidia huyo asiye na uwezo!Jinsi ulivyouokoa mkono usio na nguvu!
3. Jinsi ulivyomshauri huyo asiye na hekima!Na kutangaza ujuzi wa kweli kwa wingi!
4. Je! Umetamka maneno kwa nani?Kisha ni roho ya nani iliyotoka kwako?
5. Hao waliokufa watetemaChini ya maji na hao wayakaao.
6. Kaburi li wazi mbele yake,Uharibifu nao hauna kifuniko.
7. Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu,Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu.