Ayu. 24:8-12 Swahili Union Version (SUV)

8. Hutota kwa manyunyo ya milimani,Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,

9. Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba,Na kutwaa rehani kwa maskini;

10. Hata wazunguke uchi pasipo mavazi,Nao wakiwa na njaa huchukua miganda;

11. Hushindika mafuta ndani ya makuta ya watu hao;Wakanyaga mashinikizo, nao wana kiu.

12. Watu huugua toka mji ulio na watu wengi,Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele;Wala Mungu hauangalii upumbavu.

Ayu. 24