8. Hutota kwa manyunyo ya milimani,Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,
9. Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba,Na kutwaa rehani kwa maskini;
10. Hata wazunguke uchi pasipo mavazi,Nao wakiwa na njaa huchukua miganda;
11. Hushindika mafuta ndani ya makuta ya watu hao;Wakanyaga mashinikizo, nao wana kiu.
12. Watu huugua toka mji ulio na watu wengi,Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele;Wala Mungu hauangalii upumbavu.