1. Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi?Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?
2. Wako waziondoao alama za mipaka;Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.
3. Humfukuza punda wake asiye baba,Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.
4. Humgeuza mhitaji aiache njia;Maskini wa nchi hujificha pamoja.
5. Tazama, kama punda-mwitu jangwaniWao hutoka kwenda kazini mwao, wakitafuta chakula kwa bidii;Jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
6. Hukata nafaka zao mashambani;Na kuokota zabibu za waovu.
7. Hujilaza usiku kucha uchi pasipo nguo,Wala hawana cha kujifunika baridi.
8. Hutota kwa manyunyo ya milimani,Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,