Ayu. 24:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi?Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?

2. Wako waziondoao alama za mipaka;Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.

3. Humfukuza punda wake asiye baba,Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.

4. Humgeuza mhitaji aiache njia;Maskini wa nchi hujificha pamoja.

Ayu. 24