Ayu. 23:5-10 Swahili Union Version (SUV)

5. Ningeyajua maneno atakayonijibu,Na kuelewa na hayo atakayoniambia.

6. Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake?La, lakini angenisikiliza.

7. Hapo walekevu wangepata kuhojiana naye;Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele.

8. Tazama, naenda mbele, wala hayuko;Narudi nyuma, lakini siwezi kumwona;

9. Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona;Hujificha upande wa kuume, hata nisimwone.

10. Lakini yeye aijua njia niendeayo;Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

Ayu. 23