Ayu. 22:23-28 Swahili Union Version (SUV)

23. Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa;Ukiuondoa udhalimu mbali na hema yako.

24. Nawe hazina zako ziweke mchangani,Na dhahabu ya Ofiri iweke kati ya mawe ya vijito;

25. Naye Mwenyezi atakuwa hazina yako,Atakuwa ni fedha ya thamani kwako.

26. Kwani ndipo utakapojifurahisha katika Mwenyezi,Na kuinua uso wako kumwelekea Mungu.

27. Utamwomba yeye naye atakusikia;Nawe utazitimiliza nadhiri zako.

28. Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako;Na mwanga utaziangazia njia zako.

Ayu. 22