23. Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa;Ukiuondoa udhalimu mbali na hema yako.
24. Nawe hazina zako ziweke mchangani,Na dhahabu ya Ofiri iweke kati ya mawe ya vijito;
25. Naye Mwenyezi atakuwa hazina yako,Atakuwa ni fedha ya thamani kwako.
26. Kwani ndipo utakapojifurahisha katika Mwenyezi,Na kuinua uso wako kumwelekea Mungu.
27. Utamwomba yeye naye atakusikia;Nawe utazitimiliza nadhiri zako.
28. Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako;Na mwanga utaziangazia njia zako.