Ayu. 22:18-23 Swahili Union Version (SUV)

18. Naye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vyema;Lakini mashauri ya waovu na yawe mbali nami.

19. Wenye haki huyaona hayo wakafurahi;Nao wasio na hatia huwacheka;

20. Wasema, Hakika hao waliotuinukia wamekatiliwa mbali,Na mabaki yao moto umeyateketeza.

21. Mjue sana Mungu, ili uwe na amani;Ndivyo mema yatakavyokujia.

22. Uyapokee, tafadhali, mafunzo yatokayo kinywani mwake,Na maneno yake yaweke moyoni mwako.

23. Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa;Ukiuondoa udhalimu mbali na hema yako.

Ayu. 22