12. Huimba kwa matari na kwa kinubi,Na kuifurahia sauti ya filimbi.
13. Siku zao hutumia katika kufanikiwa,Kisha hushuka kuzimuni ghafula.
14. Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee;Kwani hatutaki kuzijua njia zako.
15. Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie?Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?
16. Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao;Mashauri ya waovu na yawe mbali nami.
17. Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimishwa?Na msiba wao kuwajilia?Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake?