7. Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi;Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
8. Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita,Na kutia giza katika mapito yangu.
9. Amenivua utukufu wangu,Na kuiondoa taji kichwani mwangu.
10. Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka;Na tumaini langu ameling’oa kama mti.
11. Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu,Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake.