1. Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2. Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini,Na kunivunja-vunja kwa maneno?
3. Mara kumi hizi mmenishutumu;Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.
4. Ingawaje nimekosa,Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.
5. Kwamba mtajitukuza juu yangu,Na kunena juu yangu shutumu langu;