Ayu. 16:5-15 Swahili Union Version (SUV)

5. Lakini ningewatia nguvu kwa kinywa changu,Na utuzo wa midomo yangu ungetuliza.

6. Nijapokuwa nanena, huzuni yangu haitulizwi;Nijapokuwa najizuia, nimepunguziwa kitu gani?

7. Lakini sasa amenichokesha;Jamii yangu yote umeifanya ukiwa.

8. Umenishika sana, ni ushahidi juu yangu;Na kukonda kwangu kwaniinukia, kwanishuhudia usoni pangu.

9. Amenirarua katika ghadhabu zake, na kunionea;Amesaga-saga meno juu yangu;Mtesi wangu hunikazia macho makali.

10. Wamenifumbulia vinywa vyao;Wamenipiga shavuni kwa kunitukana;Hujikutanisha pamoja juu yangu.

11. Mungu amenitia kwa hao wapotovu,Na kunitupa mikononi mwao waovu.

12. Nilikuwa katika raha, naye akanivunja-vunja;Naam, amenishika shingo, na kuniponda;Tena amenisimamisha niwe shabaha yake.

13. Wapigaji wake wa mishale hunizingira kotekote,Hunipasua viuno vyangu, asinihurumie;Nyonga zangu amezimwaga juu ya nchi.

14. Hunivunja kwa uvunjifu juu ya uvunjifu;Hunishambulia mfano wa jitu shujaa.

15. Nimeshona nguo ya magunia juu ya mwili wangu,Na pembe yangu nimeidhili uvumbini.

Ayu. 16