5. Lakini ningewatia nguvu kwa kinywa changu,Na utuzo wa midomo yangu ungetuliza.
6. Nijapokuwa nanena, huzuni yangu haitulizwi;Nijapokuwa najizuia, nimepunguziwa kitu gani?
7. Lakini sasa amenichokesha;Jamii yangu yote umeifanya ukiwa.
8. Umenishika sana, ni ushahidi juu yangu;Na kukonda kwangu kwaniinukia, kwanishuhudia usoni pangu.
9. Amenirarua katika ghadhabu zake, na kunionea;Amesaga-saga meno juu yangu;Mtesi wangu hunikazia macho makali.
10. Wamenifumbulia vinywa vyao;Wamenipiga shavuni kwa kunitukana;Hujikutanisha pamoja juu yangu.
11. Mungu amenitia kwa hao wapotovu,Na kunitupa mikononi mwao waovu.
12. Nilikuwa katika raha, naye akanivunja-vunja;Naam, amenishika shingo, na kuniponda;Tena amenisimamisha niwe shabaha yake.
13. Wapigaji wake wa mishale hunizingira kotekote,Hunipasua viuno vyangu, asinihurumie;Nyonga zangu amezimwaga juu ya nchi.
14. Hunivunja kwa uvunjifu juu ya uvunjifu;Hunishambulia mfano wa jitu shujaa.
15. Nimeshona nguo ya magunia juu ya mwili wangu,Na pembe yangu nimeidhili uvumbini.