5. Kwani uovu wako unakufundisha kinywa chako,Nawe wachagua ulimi wake mwenye hila.
6. Kinywa chako mwenyewe chakuhukumia makosa, wala si mimi;Naam, midomo yako mwenyewe hushuhudia juu yako.
7. Je! Wewe u mtu wa kwanza aliyezaliwa?Au, ulizawa wewe kabla ya milima?
8. Je! Umesikia mashauri ya siri ya Mungu?Nawe je! Wazuia hekima iwe yako tu?
9. Je! Wewe wajua neno lipi, ambalo sisi hatulijui?Nawe wafahamu nini, ambalo halimo ndani yetu?
10. Wenye mvi, na walio wazee sana, wote wapo pamoja nasi,Ambao ni wazee kuliko baba yako.
11. Je! Utulizi wa Mungu ni mdogo sana kwako,Na hilo neno la upole si kitu kwako?
12. Mbona moyo wako unakutaharakisha!Na macho yako, je! Kwani kung’ariza?
13. Hata ukageuza roho yako iwe kinyume cha Mungu,Na kuyatoa maneno kama hayo kinywani mwako.
14. Je! Mwanadamu ni kitu gani, hata akawa safi?Huyo aliyezaliwa na mwanamke, hata awe na haki?
15. Yeye hawategemei watakatifu wake;Naam, mbingu nazo si safi machoni pake.
16. Sembuse mtu ambaye ni mwenye kuchukiza na uchafu,Mwanadamu anywaye uovu kama anywavyo maji!
17. Mimi nitakuonyesha, unisikilize;Na hayo yote niliyoyaona nitayanena;
18. (Ambayo watu wenye hekima wameyatangazaTokea baba zao, wala hawakuyaficha;
19. Waliopewa hiyo nchi peke yao,Wala mgeni hakupita kati yao);
20. Mtu mwovu huwa na uchungu siku zake zote,Hata hesabu ya miaka aliyowekewa mwenye kuonea.