26. Humshambulia na shingo ngumu,Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;
27. Kwa kuwa amefunika uso wake na kunona kwake,Na kuwandisha mafuta kiunoni mwake;Naye amekaa katika miji iliyo ukiwa,
28. Katika nyumba ambazo hapana mtu azikaaye,Zilizokuwa tayari kuwa magofu.
29. Hatakuwa tajiri, wala mali zake hazitadumu,Wala maongeo yao hayatainama nchi.
30. Hataondoka gizani;Ndimi za moto zitayakausha matawi yake,Naye ataondoka kwa pumzi za kinywa chake.
31. Asiutumainie ubatili, na kujidanganya;Kwa kuwa huo ubatili ndio utakaokuwa ujira wake.
32. Jambo hili litatendeka kabla ya wakati wake,Na tawi lake halitasitawi.
33. Atayapukutisha mapooza yake kama mzabibu,Na kuyatupa maua yake kama mzeituni.