Ayu. 15:21-26 Swahili Union Version (SUV)

21. Sauti za utisho zi masikioni mwake;Katika kufanikiwa kwake mtekaji nyara atamjia juu yake;

22. Yeye hasadiki kwamba atarudi kutoka gizani,Naye hungojewa na upanga;

23. Hutanga-tanga ili apate chakula, akisema, Ki wapi?Ajua kwamba siku ya giza i tayari karibu yake;

24. Mateso na dhiki humtia hofu;Humshinda kama vile mfalme aliye tayari kwa vita;

25. Kwa kuwa amenyosha mkono wake juu ya Mungu,Na kuendelea kwa kiburi kinyume cha Mwenyezi;

26. Humshambulia na shingo ngumu,Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;

Ayu. 15