2. Je! Yapasa mtu mwenye hekima kujibu kwa ujuzi wa uvuvio,Na kujaza tumbo lake na upepo wa mashariki?
3. Je! Ahoji na mazungumzo yasiyo faida,Au kwa maneno ambayo hawezi kufanya mema kwayo?
4. Naam, wewe waondoa kicho,Nawe wazuia ibada mbele za Mungu.
5. Kwani uovu wako unakufundisha kinywa chako,Nawe wachagua ulimi wake mwenye hila.
6. Kinywa chako mwenyewe chakuhukumia makosa, wala si mimi;Naam, midomo yako mwenyewe hushuhudia juu yako.
7. Je! Wewe u mtu wa kwanza aliyezaliwa?Au, ulizawa wewe kabla ya milima?
8. Je! Umesikia mashauri ya siri ya Mungu?Nawe je! Wazuia hekima iwe yako tu?