Ayu. 13:18-23 Swahili Union Version (SUV)

18. Angalieni sasa, nimekwisha kulitengeneza neno langu,Najua ya kuwa ni mwenye haki mimi.

19. Yuko nani atakayeshindana nami?Maana sasa nitanyamaa kimya na kutoa roho.

20. Lakini msinifanyie mambo mawili, hayo tu,Ndipo nami sitajificha usoni pako;

21. Uondoe mkono wako usinilemee;Na utisho wako usinitie hofu.

22. Basi uite wakati huo, nami nitaitika;Au, niache ninene mimi, nawe unijibu.

23. Maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi?Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.

Ayu. 13