21. Humwaga aibu juu ya hao wakuu,Na kulegeza mshipi wa wenye nguvu.
22. Huvumbua mambo ya siri tokea gizani,Na hicho kilicho giza tupu huleta mwangani.
23. Huyaongeza mataifa, na kuyaangamiza;Huyaeneza mataifa mbali, na kuyaacha.
24. Huwaondolea moyo wakuu wa watu wa nchi,Na kuwapoteza nyikani pasipokuwa na njia.
25. Wao hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga,Naye huwafanya kupepesuka kama vile mlevi.