1. Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu, na kusema,
2. Je! Huu wingi wa maneno usijibiwe?Na mtu aliyejaa maneno, je! Ahesabiwe kuwa na haki?
3. Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya?Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha?
4. Kwa kuwa wewe wasema, Mafunzo yangu ni safi,Nami ni safi machoni pako.