4. Je! Wewe una macho ya kimwili,Au je! Waona kama aonavyo binadamu?
5. Je! Siku zako ni kama siku za mtu,Au je! Miaka yako ni kama siku za mtu,
6. Hata ukauliza-uliza habari za uovu wangu,Na kuitafuta dhambi yangu,
7. Ujapojua ya kuwa mimi si mwovu;Wala hapana awezaye kuokoa na mkono wako?
8. Mikono yako imeniumba na kunifinyanga;Nawe utageuka na kuniangamiza?