Amu. 8:17-19 Swahili Union Version (SUV)

17. Kisha akaupomosha mnara wa Penieli, na kuwaua watu wa mji huo.

18. Ndipo akawaambia hao Zeba na Salmuna, Hao watu mliowaua huko Tabori walikuwa watu wa namna gani? Wakamjibu, Walikuwa kama wewe ulivyo; kila mmoja alikuwa anafanana na wana wa mfalme.

19. Naye akasema, Watu hao walikuwa ndugu zangu, wana wa mamaangu mimi; kama yeye BWANA alivyo hai, kwamba mliwaokoa hai watu hao, mimi nisingewaua ninyi.

Amu. 8