6. Katika siku za Shamgari, mwana wa Anathi,Siku za Yaeli, njia kuu zilikuwa hazina watu;Nao wenye kusafiri walipita kwa njia za kando.
7. Maliwali walikoma katika Israeli, walikoma,Hata mimi Debora nilipoinuka,Nilipoinuka mimi, mama katika Israeli.
8. Walichagua miungu mipya,Ndipo kulikuwa na vita malangoni;Je! Ilionekana ngao au mkukiKatika watu elfu arobaini wa Israeli?
9. Moyo wangu unawaelekea maliwali wa Israeli,Waliojitoa nafsi zao kwa hiari yao miongoni mwa watu;Mhimidini BWANA.