Amu. 5:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ndipo Debora, na Baraka mwana wa Abinoamu, wakaimba siku ile, wakisema;

2. Kwa sababu wakuu walitangulia katika Israeli,Kwa sababu watu walijitoa nafsi zao kwa hiari yao,Mhimidini BWANA.

3. Sikieni, enyi wafalme; tegeni masikio, enyi wakuu;Mimi, naam mimi, nitamwimbia BWANA;Nitamhimidi BWANA, Mungu wa Israeli.

4. BWANA, ulipotoka katika Seiri,Ulipokwenda vitani kutoka mashamba ya Edomu,Nchi ilitetema, mbingu nazo zikadondoza maji,Naam, mawingu yakadondoza maji.

Amu. 5