2 Sam. 23:5-11 Swahili Union Version (SUV)

5. Je! Sivyo ilivyo nyumba yangu mbele za BWANA?Kwa kuwa amefanya nami agano la milele;Ina taratibu katika yote, ni thabiti,Maana ni wokovu wangu wote, na shauku langu lote.

6. Lakini hatawachipuza watu wa ubatili;Watakuwa wote kama miiba ya nyikani ya kutupwa,Ambayo haivuniki kwa mkono,

7. Mtu atakayeigusa hiyo,Na awe na chuma na mpini wa mkuki,Nao watateketezwa papo hapo kwa moto.

8. Haya ndiyo majina ya mashujaa aliokuwa nao Daudi; Yashobeamu Mhakmoni, mkuu wa maakida; huyo aliliinua shoka lake juu ya watu mia nane waliouawa pamoja.

9. Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao;

10. huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye BWANA akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu.

11. Na baada yake kulikuwa na Shama, mwana wa Agee, Mharari; nao Wafilisti walikuwa wamekusanyika huko Lehi, palipokuwapo konde lililojaa midengu; nao watu wakawakimbia Wafilisti;

2 Sam. 23