1. Basi haya ndiyo maneno ya mwisho ya Daudi.Daudi, mwana wa Yese, anena,Anena huyo mtu aliyeinuliwa juu,Yeye, masihi wake Mungu wa Yakobo,Mtungaji wa nyimbo za Israeli mwenye kupendeza;
2. Roho ya BWANA ilinena ndani yangu,Na neno lake likawa ulimini mwangu.
3. Mungu wa Israeli alisema,Mwamba wa Israeli aliniambia,Atawalaye wanadamu kwa haki,Akitawala katika kicho cha Mungu,
4. Atakuwa kama nuru ya asubuhi jua lichapo,Asubuhi isiyo na mawingu.Lachipuza majani mabichi juu ya nchi,Kwa mwangaza baada ya mvua;