2 Sam. 1:21-24 Swahili Union Version (SUV)

21. Enyi milima ya Gilboa, visiwepo juu yenuUmande wala mvua, wala mashamba ya matoleo;Maana ndipo ilipotupwa kwa aibu ngao ya shujaa,Ngao yake Sauli, pasipo kutiwa mafuta.

22. Kutoka kwa damu yao waliouawa,Kutoka kwa shahamu yao mashujaa,Upinde wa Yonathani haukurudi nyuma,Wala upanga wa Sauli haukurudi bure.

23. Sauli na Yonathani walipendwa na kupendezaMaishani wala mautini hawakutengwa;Walikuwa wepesi kuliko tai,Walikuwa hodari kuliko simba.

24. Enyi binti za Israeli, mlilieniHuyo Sauli, ambaye aliwavikaMavazi mekundu kwa anasa,Akazipamba nguo zenu dhahabu.

2 Sam. 1