1. Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala; akatawala miaka arobaini huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Sibia wa Beer-sheba.
2. Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa BWANA siku zote za Yehoyada kuhani.
3. Yehoyada akamwoza wake wawili, naye akazaa wana na binti.