2 Nya. 24:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala; akatawala miaka arobaini huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Sibia wa Beer-sheba.

2. Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa BWANA siku zote za Yehoyada kuhani.

3. Yehoyada akamwoza wake wawili, naye akazaa wana na binti.

2 Nya. 24