2 Nya. 12:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Akaitwaa miji yenye maboma iliyokuwa ya Yuda, akaja Yerusalemu.

5. Ndipo akaja Shemaya nabii kwa Rehoboamu, na kwa wakuu wa Yuda, waliokusanyika Yerusalemu kwa sababu ya Shishaki, akawaambia, BWANA asema hivi, Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo nami nimewaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.

6. Ndipo wakajinyenyekeza wakuu wa Israeli na mfalme; wakasema, BWANA ndiye mwenye haki.

7. Naye BWANA alipoona ya kwamba wamejinyenyekeza, neno la BWANA likamjia Shemaya, kusema, Wamejinyenyekeza; sitawaharibu; lakini nitawapa wokovu punde, wala ghadhabu yangu haitamwagika juu ya Yerusalemu kwa mkono wa Shishaki.

8. Walakini watamtumikia; ili wapate kujua utumwa wangu, na huo utumwa wa falme za nchi.

2 Nya. 12