4. BWANA asema hivi, Hamtapanda wala kupigana na ndugu zenu; rudini kila mtu nyumbani kwake; kwa kuwa jambo hili limetoka kwangu. Basi, wakayasikiliza maneno ya BWANA, wakarudi katika kumwendea Yeroboamu.
5. Naye Rehoboamu akakaa Yerusalemu, akajenga miji yenye ngome katika Yuda.
6. Akajenga na Bethlehemu, na Etamu, na Tekoa,
7. na Bethsuri, na Soko, na Adulamu,
8. na Gathi, na Maresha, na Zifu,
9. na Adoraimu, na Lakishi, na Azeka,