2 Fal. 17:37-41 Swahili Union Version (SUV)

37. na sheria, na hukumu, na torati, na amri, alizowaandikia, hizo ndizo mtakazozishika na kuzifanya hata milele; wala msiche miungu mingine.

38. Na hilo agano nililofanya nanyi, msilisahau; wala msiche miungu mingine;

39. lakini BWANA, Mungu wenu, ndiye mtakayemcha; naye atawaokoa mikononi mwa adui zenu wote.

40. Walakini hawakusikia, bali wakafanya sawasawa na kawaida zao za kwanza.

41. Basi mataifa hawa wakamcha BWANA, tena wakaziabudu sanamu zao za kuchongwa; na wana wao vile vile, na wana wa wana wao; kama walivyofanya baba zao, wao nao hufanya vivyo hivyo hata leo.

2 Fal. 17