1 Tim. 5:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai.

7. Mambo hayo pia uyaagize, ili wasiwe na lawama.

8. Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

9. Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja;

10. naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema.

1 Tim. 5