1 Tim. 4:8-11 Swahili Union Version (SUV)

8. Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.

9. Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa;

10. kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio.

11. Mambo hayo uyaagize na kuyafundisha.

1 Tim. 4