1 Tim. 3:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.

2. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;

3. si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;

4. mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;

5. (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)

6. Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.

1 Tim. 3