15. Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
16. Furahini siku zote;
17. ombeni bila kukoma;
18. shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.
19. Msimzimishe Roho;
20. msitweze unabii;
21. jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;
22. jitengeni na ubaya wa kila namna.
23. Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24. Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.