1 The. 5:11-21 Swahili Union Version (SUV)

11. Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.

12. Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni;

13. mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.

14. Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.

15. Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.

16. Furahini siku zote;

17. ombeni bila kukoma;

18. shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.

19. Msimzimishe Roho;

20. msitweze unabii;

21. jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;

1 The. 5