1 The. 4:4-10 Swahili Union Version (SUV)

4. kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

5. si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.

6. Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosa katika jambo hili; kwa sababu Bwana ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana.

7. Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.

8. Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali Mungu, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.

9. Katika habari ya upendano, hamna haja niwaandikie; maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana.

10. Kwa maana mnafanya neno hili kwa ndugu wote walio katika Makedonia yote. Lakini twawasihi, ndugu, mzidi sana.

1 The. 4