1 Sam. 8:3-5 Swahili Union Version (SUV)

3. Ila wanawe hawakuenda katika njia zake, bali waliziacha, ili wapate faida; wakapokea rushwa, na kupotosha hukumu.

4. Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samweli huko Rama;

5. wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote.

1 Sam. 8