1 Sam. 2:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Naye Hana akaomba, akasema,Moyo wangu wamshangilia BWANA,Pembe yangu imetukuka katika BWANA,Kinywa changu kimepanuka juu ya adui zangu;Kwa kuwa naufurahia wokovu wako;

2. Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA;Kwa maana hakuna ye yote ila wewe,Wala hakuna mwamba kama Mungu wetu.

3. Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo;Majivuno yasitoke vinywani mwenu;Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa,Na matendo hupimwa na yeye kwa mizani.

4. Pinde zao mashujaa zimevunjika,Na hao waliojikwaa wamefungiwa nguvu.

5. Walioshiba wamejikodisha ili kupata chakula,Na hao waliokuwa na njaa wamepata raha.Naam, huyo aliyekua tasa amezaa watoto saba,Na yeye aliye na wana wengi amedhoofika.

1 Sam. 2