1 Sam. 1:26-28 Swahili Union Version (SUV)

26. Akasema, Ee bwana wangu, kama iishivyo roho yako, bwana wangu, mimi ndimi yule mwanamke aliyesimama karibu nawe hapa, nikimwomba BWANA.

27. Naliomba nipewe mtoto huyu; BWANA akanipa dua yangu niliyomwomba;

28. kwa sababu hiyo mimi nami nimempa BWANA mtoto huyu; wakati wote atakaokuwa hai amepewa BWANA. Naye akamwabudu BWANA huko.

1 Sam. 1