1 Pet. 4:5-11 Swahili Union Version (SUV)

5. Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.

6. Maana kwa ajili hiyo hata hao waliokufa walihubiriwa Injili, ili kwamba wahukumiwe katika mwili kama wahukumiwavyo wanadamu; bali wawe hai katika roho kama Mungu alivyo hai.

7. Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.

8. Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.

9. Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung’unika;

10. kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.

11. Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.

1 Pet. 4