1 Nya. 23:30-32 Swahili Union Version (SUV)

30. nao wasimame kila asubuhi kumshukuru na kumsifu BWANA, na jioni vivyo hivyo;

31. na kumtolea BWANA sadaka zote za kuteketezwa, katika siku za sabato, za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoagizwa, kwa hesabu kadiri ya agizo lake, daima mbele za BWANA;

32. tena walinde ulinzi wa hema ya kukutania, na ulinzi wa patakatifu, na ulinzi wa wana wa Haruni, ndugu zao, katika utumishi wa nyumba ya BWANA.

1 Nya. 23