1 Nya. 2:38-44 Swahili Union Version (SUV)

38. na Obedi akamzaa Yehu; na Yehu akamzaa Azaria;

39. na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa

40. na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu;

41. na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.

42. Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni.

43. Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema.

44. Naye Shema akamzaa Rahamu, babaye Yorkeamu; na Rekemu akamzaa Shamai.

1 Nya. 2