1 Nya. 16:10-16 Swahili Union Version (SUV)

10. Jisifuni kwa jina lake takatifu;Na ufurahi moyo wao wamtafutao BWANA.

11. Mtakeni BWANA na nguvu zake;Utafuteni uso wake siku zote.

12. Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya;Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;

13. Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake,Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

14. Yeye, BWANA, ndiye Mungu wetu;Duniani mwote mna hukumu zake.

15. Likumbukeni agano lake milele,Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.

16. Agano alilofanya na Ibrahimu,Na uapo wake kwa Isaka;

1 Nya. 16