1 Nya. 12:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. na Ishmaya Mgibeoni, shujaa wa wale thelathini, naye alikuwa juu ya wale thelathini; na Yeremia, na Yahazieli, na Yohana, na Yozabadi Mgederathi;

5. Eluzai, na Yerimothi, na Bealia, na Shemaria, na Shefatia Mharufi;

6. Elkana, na Ishia, na Azaleli, na Yoezeri, na Yashobeamu, Wakora;

7. na Yoela, na Zebadia, wana wa Yerohamu, wa Gedori.

8. Na wa Wagadi wakajitenga kumfuata Daudi ngomeni huko nyikani, waume mashujaa, watu waliozoea vita, walioweza kutumia ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kama nyuso za simba, nao walikuwa wepesi kama kulungu juu ya milima;

1 Nya. 12