1 Kor. 15:33-38 Swahili Union Version (SUV)

33. Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.

34. Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.

35. Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?

36. Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;

37. nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;

38. lakini Mungu huipa mwili kama apendavyo, na kila mbegu mwili wake.

1 Kor. 15